HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania yashiriki kikamilifu maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani

 








Wanawake watumishi kutoka Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania wameshiriki maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani ambapo kimkoa yamefanyika katika viwanja vya Chinangari Park Jijini Dodoma.  

 Akizungumza mara baada ya maadhimisho hayo leo Machi 8,2025 Afisa Ugavi wa Tume hiyo Bi. Aneth Lyatuu amesema kuwa siku ya leo inawakumbusha na kuwapa ujasiri zaidi wa kuweza kusimamia malengo ambayo wamejiwekea katika akili zao. 

  "Siku ya leo niwaambie wanawake wenzangu tujitahidi kupendana ,mwenzako akikukasirisha mwambie, msamehe na tusonge mbele pia tutiane moyo na nguvu,"amesema.  

 Aidha amesema kupitia maadhimisho hayo wanawake wasisahau maadili ya watoto kwasababu wanawake ndiyo wanaoongoza jamii na inaanzia katika familia na wakisimama imara jamii yote itaimarika. 

  Maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani kitaifa yamefanyika Jijini Arusha ambapo yameongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Mtazamo wa Jaji Winifrida Korosso kufuatia Maadhimisho ya wiki ya Sheria

JAJI WINIFRADA KOROSSO ATEMBELEA UWANJA WA MAADHIMISHO YA SIKU YA SHERIA...

PROF. ELISANTE OLE GABRIEL ATEMBELEA BANDA LA TUME YA KUREKEBISHA SHERI...

Mabaraza ya wafanyakazi yatumike Kujenga Demokrasia sehemu za kazi - Kabudi



Mabaraza ya  wafanyakazi yanapaswa kutumika kama chombo muhimu katika kuboresha na kuimarisha demokrasia kwenye eneo la kazi badala ya kutumika pekee kukusanya na  kupitia maoni ya watumishi .


Kauli hiyo imetolewa tarehe 14/11/2024 na Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi katika ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Midland iliyopo mjini Dodoma wakati akifungua kikao cha 21 cha baraza la wafanyakazi la Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania ambapo ameleleza mabaraza hayo  yanahusisha ushirikishwaji wa wafanyakazi katika maamuzi ya Taasisi au shirika wanamofanyia kazi jambo ambalo  huongeza uwazi na uwajibikaji.

Waziri Kabudi ameipongeza Manejimenti ya Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania kwa kutimiza takwa la kisheria la kufanya kikao cha baraza huku akifafanua kwamba Baraza la Wafanyakazi halipaswi kuwa chombo cha kupokea malalamiko ya watumishi pekee ingawa ni muhimu kwa baraza hilo kushughulikia malalamiko na changamoto zinazowakabili wafanyakazi na badala yake  jukumu lake linapaswa kuwa pana zaidi. 

Prof amefafanua kwamba Baraza linaweza na linapaswa kuwa jukwaa la kuchochea maendeleo, kutoa maoni, na kutoa mawazo ya kuboresha ufanisi wa Taasisi kwa ujumla.

Demokrasia  katika eneo la kazi ni muhimu kwani inachochea ari ya kazi, kuimarisha ufanisi, na kujenga mazingira yenye amani na haki, alisistiza Waziri wa Kabudi.

“ Baraza la Wafanyakazi si tu chombo cha kusimamia haki za wafanyakazi, bali pia ni nyenzo muhimu ya kufanikisha malengo ya taasisi kupitia ushirikiano wa kweli na mawasiliano ya wazi” alisema Waziri 

Amesema  Baraza linatoa nafasi kwa wafanyakazi kutoa maoni, mawazo, na mapendekezo kuhusu masuala yanayohusu ustawi wao na maendeleo ya Taasisi kwa ujumla  hivyo kupitia Baraza la Wafanyakazi, viongozi watakiwa  kupata mawazo mapya ya kuboresha mazingira ya kazi.

Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa Tume hiyo Bw. George Mandepo, alieleza kwamba kikao hicho ni hitaji la kisheria na ni muhimu kwa kuwa linashirikisha  wafanyakazi katika michakato ya kufanya maamuzi ili kuimarisha ufanisi wa kazi.


Aidha amefafanua kwamba Tume inatekeleza mipango mbalimbali ya kuhakikisha kwamba watumishi wanapata mafunzo  ili kuwajengea uwezo na kuboresha ufanisi  katika kutekeleza majukumu yao.

Mkutano huo uliwaleta pamoja wafanyakazi wa Tume na wadau wengine muhimu kwa lengo la kujadili masuala ya kazi, kubadilishana mawazo, na kutafuta suluhisho la changamoto zinazokabili sekta ya sheria.


MWISHO

WAASISI WALIVYO ELEZEA HISTORIA YA TUME YA KUREKEBISHA SHERIA TANZANIA

Mkakati wa Elimu kwa Umma Ulivyo Wakosha Kanda ya Kaskazini Kuhusu Sheria ya Mapato Yatokanayo na Uhalifu.




Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT) imetoa elimu kuhusu dhana ya mapato yatokanayo na uhalifu, ambayo inahusu mali, fedha, au faida zinazopatikana kutokana na vitendo vya kihalifu.

Wakitoa mada hiyo katika kituo cha redio cha Banana Fm na Redio five ya Mkoani moshi na Arusha   Mawakili  wa Serikali Anjela Mnzava Shila na Vicky Mbunde kutoka Tume hiyo wamesema lengo la   elimu hiyo ni kuhakikisha jamii inaelewa kuwa mali zote zinazopatikana kupitia njia zisizo halali zinaweza kuchukuliwa na serikali kupitia taratibu za kisheria ili kudhibiti uhalifu na kupunguza motisha kwa wananchi wa kushiriki katika vitendo vya kihalifu.

Wakili wa serikali Anjela Shilla akielezea maana ya mapato ya uhalifu alisema ni mapato au mali yoyote itokanayo na uhalifu ambapo alibainisha kwamba  suala la mapato yatokanayo na uhalifu ni mtambuka kwa kuwa  linalogusa sheria mbalimbali kama vile Sheria ya Mapato Yatokanayo na Uhalifu, Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa , Sheria ya Kuzuia Utakasishaji wa Fesha Haramu, Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, Sheria ya Wanyamapori, na Sheria ya Kuzuia Usafirishaji Haramu wa Binadamu. Sheria hizi zimeelezea namna ya utaifishaji wa mali zitokanazo na uhalifu kwa Nia ya kuzuia uhalifu na kufundisha jamii kuwa uhalifu haulipi.



Aidha Shila ameeleza kwamba  elimu hiyo inahusisha kuwaelimisha wananchi na taasisi za fedha juu ya mbinu zinazotumika kuficha mazao ya uhalifu, kama vile utakatishaji wa fedha, na umuhimu wa kutoa taarifa wanapoona shughuli za kutiliwa shaka.

Kwa upande wake Wakili Vicky Mbunde   amefafanua kwamba  zipo sheria ambazo  zinazohusika na kusimamia mapato yatokanayo na uhalifu ambazo zinalenga kudhibiti, kuchunguza, na kutaifisha mali au fedha zinazopatikana kupitia vitendo vya kihalifu.

Tanzania kama nchi mwanachama wa mikataba mbalimbali ya nje ya nchi imesaini Mkataba wa Umoja wa Mataifa Dhidi ya Uhalifu wa Kupangwa Unaovuka Mipaka na Mkataba wa Umoja wa Mataifa Dhidi ya Rushwa unaotaka nchi wanachama kuweka Mifumo dhabiti ya kisheria ya Kupambana na Uhalifu