HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

» » WATUMISHI WA TUME YA KUREKEBISHA SHERIA WAPATA CHANJO YA HOMA YA INNI

 



Katibu Mtendaji wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanznaia Griffin Mwakapeje amewataka watumishi wote wa Tume hiyo ambao hawajapata chanjo ya homa ya inn kutumia nafasi ya Uwepo wa wataalamu wa afya ofisini hapo kupata chanjo hiyo itakayotolewa kwa muda wa siku moja ya tarehe 15.08.2023

Akiongea leo baada  ya kuwapokea wataalamu hao kutoka Wizara ya Afya nchini ambao wanatoa chanjo ya Inni kwa gharama za ofisi amesema ni fursa kwa kila Mtumishi kupata chanjo hiyo kama alikuwa hajapata.

Aidha amesema ili watumishi waweze kutekeleza majukumu yao vizuri ni lazima wawe na afya nzuri  hivyo kila mtumishi anatakiwa kutimiza jukumu hilo kwa kuwaona wataalamu hao.

Huduma hiyo ya chanjo inapatikana katika ofisi za Tume zilizopo Chuo kikuu cha Dodoma katika offisi namba 301 ghorofa ya tatu

Awali wataalamu hao walisema kwamba dalili za ugojwa huo ni   Kutapika, kuhara au maumivu ya tumbo,   Rangi ya manjano kwenye macho na ngozi pamoja na mtu kupata choo kilicho na rangi ya mpauko.

Kwa kawaida, homa kali ya ini inaweza kupona bila hata madhara ya hapo kwa hapo Katika baadhi ya wagonjwa, maambukizi ya homa kali ya ini aina B au C yanaweza kusababisha maambukizi sugu na kusababisha kovu, ini kushindwa kufanya kazi au hata saratani. Homa kali ya ini inakuwa mbaya zaidi kwa watu wazima kuliko watoto. Watu wazima huonesha zaidi dalili za ugonjwa kuliko watoto na madhara makubwa zaidi ya ugonjwa huo ni kwa watu wenye umri mkubwa’walisema

 

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Tuandikie Maoni yako