HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

UTAFITI NI NJIA YA UHAKIKA YA KUWEZESHA KUWA NA SHERIA MADHUBUTI NA ZENYE TIJA KWA TAIFA- MANDEPO

 


Katibu Mtendaji Tume ya Kufekebisha Sheria Tanzania Bw. George Nathaniel Mandepo amesema kuwa utafiti ni mbinu  muhimu inayoweza kusaidia Serikali  kuamua kama sheria au iboreshwe au ifutwe ili kuendana na mahitaji halisi ya  Taifa kwa wakati husika. 

Akizungumza katika kipindi cha Morning Trumpet cha Azam Tv kinachorushwa kila siku asubuhi kiliendesha mahojiano  kuhusu maendeleo ya sheria nchini, ambapo Bw. Mandepo alisema kuwa jamii inapobadilika, ni lazima sheria nazo zibadilike kulingana na hali. Mabadiliko hayo uhususha pia matokeo ya tafiti mbalimbali za Sheria zinazofanywa na Serikali  hususan kupitia Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania. 

“Utafiti ndio unaoamua kwamba sheria itungwe, ifutwe au iboreshwe,” alisema Mandepo huku akisisitiza umuhimu wa kuihusisha Tume hiyo katika michakato muhimu ya maboresho ya sheria hapa nchini.

Alieleza kuwa tafiti husaidia kubaini changamoto zilizopo kwenye sekta husika na pia ni mbinu ambayo uhusisha  wananchi wanaweza kuguswa au kuathirika kutokana na uwepo au kukosekana kwa sheria katika mbalimbali sekta kama elimu, afya, usalama barabarani na teknolojia. Utafiti hutoa  mwanga kwa watunga sheria kuchukua hatua sahihi, yenye tija na husishi. 

Kwa mujibu wa Mandepo, baadhi ya sheria zimekuwa zikiboreshwa kutokana na mabadiliko ya kijamii na maendeleo ya sayansi na teknolojia hapa nchini.  

Alitoa mfano wa sheria za mawasiliano na matumizi ya mitandao ambazo zimekuwa zikifanyiwa marekebisho mara kwa mara kutokana na ukuaji wa teknolojia duniani.
Mathalani kwa sasa amesema,kwa maelekezo ya Serukali, Tume  hiyo  inaendelea na kazi ya utafiti wa mifumo ya sheria zinazoratibu matumizi ya Akili Ude (Artificial Intelligence ) na utatifi wa mifumo ya Sheria zinaohusu Biashara ya  Hewa Ukaa. 

Kadhalika, alieleza kuwa, miongoni mwa kazi ambazo Tume hiyo imefanya hivi karibuni ni Tathmini na Mapitio sheria za Michezo ya Kubahatisha, Sheria ya Takwimu, Sheria ya Vyama vya Ushirika, Ulinzi Mashahidi na Watoa Taarifa, Matumizi ya Shisha, Bidhaa za Tumbaku na Sigara za Kielektroniki, Sheria ya Usuluhishi  pamoja na Sheria ya Makampuni na Majina ya Biashara. Pia mapendekezo ya kuboresha Sheria yametolewa kwenye Sheria za Usafirishaji Majini na Ardhini.

Aliainisha kuwa kwenye eneo ya haki jinai, Tume hiyo imepitia na kutoa mapendekezo juu ya maboresho ya sheria kwq kuzingatia matokeo ya Tume ya Rais ya Kuangalia Mifumo ya Haki Jinai (Tume ya Hakijinai). Baadhi ya Sheria zilizotazamwa ni pamoja na Sheria za Mwenendo wa Jinai, Sheria zinazogusa dhamana na Sheria ya Uhujumu Uchumi na Uharifu wa Kupangwa. 

Alisisitiza kuwa, kutokea kuanzishwa kwake, Tume imeweza kufanya Tafiti, Tathmini na mapitio ya Mifumo ya Sheria mbalimbali na kutoa Taarifa zaidi ya 70 zilizowezesha Serikali kuboresha sekta husika kwa kutunga, kufuta au kufanya mabadiliko kwenye sheria nyingi zinazogusa nyanja za haki madai na haki jinai, ajira, mahusiano, kazi,  jamii, siasa, uchumi na maendeleo ikiwemo vivutio vya uwekezaji, mifumo ya utatuzi wa migogoro na kodi. 

Tume hiyo imeendelea kutoa Elimu kwa Umma kuhusu sheria mbalimbali kwa nia ya kuwezesha wadau kufahamu haki na wajibu wao ndani ya sheria zilizopo. 

Aidha, wadau wametakiwa kushiriki katika tafiti, tathmiji na mapitio ya sheria na kutoa maoni yao ili kusaidia kujenga sheria bora zinazolinda haki, usawa na maendeleo ya taifa.

SERIKALI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MPANGO NA BAJETI YA 2025/2026 YA LRCT- NAIBU WAZIRI.

 


  • Naibu waziri Wizara ya Katiba na Sheria Mhe. Zainabu Katimba akiongea na watumishi wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania kwenye Ukumbi wa mikutano wa Tume ya Utumishi wa  Mahakama ulioko Dodoma wakati wa Baraza la wafanyakazi  la Tume hiyo.

  • Naibu waziri Wizara ya Katiba na Sheria Mhe. Zainabu Katimba amesema Serikali inaridhishwa na utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania kwa mwaka wa fedha 2025/2026, ambapo imeendelea kufanya tafiti na mapitio ya sheria mbalimbali pamoja na kutoa elimu ya sheria kwa umma.

    Kauli hiyo ameitoa tarehe 14/05/2026 katika ukumbi wa mikutano wa Tume ya Utumishi wa Mahakama uliopo mjini Dodoma wakati wa kikao cha 24 cha Baraza la wafanyakazi wa Tume hiyo ambapo ameeleza kwamba Tume imefanya mapitio ya sheria muhimu zikiwemo Sheria ya Usuluhishi, Sura ya 15; Sheria ya Bima, Sura ya 394; na Sheria ya Bima za Vyombo vya Moto (Magari) Sura ya 169, kwa lengo la kuhakikisha zinaendana na mahitaji ya sasa ya kijamii na kiuchumi.

    Mhe. Katimba alifafanua kwamba Tume inaendelea na mapitio ya Sheria ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi, Sura ya 295, Tathmini ya utekelezaji wa sheria zinazohusu umiliki wa mali na rasilimali asilia pamoja na kufanya tafiti katika maeneo mapya kama matumizi ya Akili Unde (Artificial Intelligence), biashara ya hewa ya ukaa, adhabu ya kifo na kifungo cha maisha, na usajili wa mawakili.

    “Hatua hizi zinaonesha mchango mkubwa wa Tume katika kusaidia Serikali kuwa na sheria zinazoendana na mabadiliko ya teknolojia, uchumi na mahitaji ya wakati” alieleza Mhe. Katimba.

    “Ninapenda kutambua kwa heshima kubwa juhudi zinazoendelea kufanywa na Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania katika kutekeleza majukumu yake ya msingi ya kuishauri Serikali kuhusu maboresho ya sheria mbalimbali kwa ajili ya kuendana na mahitaji ya wakati na maendeleo ya Taifa letu” Aliendelea Kusema.

    Aidha Katika mwaka wa fedha 2025/2026, Tume imewasilisha taarifa tano (5) kwa waziri wa katiba na Sheria ambazo ni Taarifa ya Mapitio ya Sheria ya Takwimu, Sura ya 351 na Taarifa kuhusu Utafiti wa Mfumo wa Sheria Zinazosimamia Vyama vya Ushirika, za Februari,2025; Taarifa ya Mapitio ya Sheria Zinazosimamia Udhibiti wa Matumizi ya Bidhaa za Tumbaku, Shisha na Sigara za Kielektroniki, Taarifa ya Tathimini ya Utekelezaji wa Sheria ya Michezo ya Kubahatisha Nchini, Sura ya 41 na Taarifa ya Utafiti kuhusu Mfumo wa Sheria Zinazosimamia Utatuzi wa Migogoro ya Mikopo katika Benki na Taasisi za Fedha, zote za Julai, 2025.

    Awali akimkaribisha Waziri huyo, Katibu Mtendaji wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Bw. George Mandepo alisema Mkutano huo utakuwa na mada zitakazo wasilishwa kwa lengo kuongeza uelewa wa shughuli za Tume, kukuza ujuzi na uzoefu katika kuimarisha utendaji kazi ambazo ni Mada kuhusu ukamilishwaji wa Mpango Mkakati wa Tume wa miaka mitano 2026/2027 – 2030/2031; Mada kuhusu Elimu ya usimamizi wa Fedha (Financial Literacy); na Mada kuhusu Maana ya Maadili na Umuhimu wa Uadilifu katika Utumishi wa Umma.

    Aidha Bw. Mandepo alieleza kuwa mwaka wa fedha 2025/2026, Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania iliidhinishiwa na Bunge kutumia jumla ya Shilingi bilion 7.45 Kati ya fedha hizo, kiasi cha Shilingi bilion 1.775 ikiwa ni kwa ajili ya Mishahara na kiasi cha Shilingi bilion 5,627 ikiwa ni kwa ajili ya Matumizi Mengineyo.

Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Yakutana na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Zanzibar Kujadili Utekelezaji wa Mkataba wa Ushirikiano (MoU)




Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania   na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Zanzibar wakati wa kikao kazi cha kuimarisha utekelezaji wa mkataba wa makubaliano ya ushirikiano (MoU) kati ya pande hizo mbilli uliofanyika katika ofisi hizo mjini Zanzibar

Katibu Mtendaji Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania ( kushoto) akisisitiza jambo wakati wa Kikao kazi kilichofanyika Zanzibar, pembeni ni Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Zanzibar Bw. Shaaban Abdalla.
Kikao kinaendelea 













Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania   imekutana na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Zanzibar katika kikao kazi kilicholenga kuimarisha utekelezaji wa mkataba wa makubaliano ya ushirikiano (MoU) kati ya pande hizo mbili, kwa lengo la kuimarisha ushirikiano  katika mapitio, maboresho, na utafiti wa sheria zinazotekelezwa katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Kikao hicho kilichofanyika  Zanzibar na kuhudhuriwa na wajumbe kutoka Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania pamoja na maafisa waandamizi kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Zanzibar kilijadili  mafanikio yaliyopatikana tangu kutiwa saini kwa makubaliano hayo, pamoja na kuweka mikakati ya pamoja ya utekelezaji wa maeneo ya kipaumbele ya kisheria kwa kipindi kijacho.

Akizungumza katika kikao hicho, Katibu Mtendaji wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzani George Mandepo, alisema kuwa ushirikiano kati ya Tume na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Zanzibar ni muhimu katika kuimarisha mfumo wa sheria nchini kwa kuzingatia mahitaji ya pande zote mbili za Muungano.

Kupitia mkataba huu wa makubaliano, tunajenga msingi madhubuti wa kushirikiana katika kufanya tafiti za kisheria, kubadilishana uzoefu, na kuimarisha uwezo wa wataalamu wetu wa sheria kutoka pande zote mbili,alisema.

Aidha Bw. Mandepo alisema kwamba LRCT kwa mwaka wa fedha 2025/26 imejipanga kufanya tafiti mbalimbali ikiwemo utafiti wa mfumo wa sheria zinazosimamia upingaji wa maamuzi ya kiutawala mahakamani,utafiti wa mfumo wa sheria zinazosimamia usajili wa Mawakili Tanzania na utafiti wa mfumo wa sheria unaosimamia biashara ya hewa ukaa.

Bw. Mandepo amefafanua kwamba Tume  kwa sasa inaendelea kufanya mapitio ya sheria ya Bima sura ya 169, mapitio ya sheria ya Bima sura ya 394 na mapitio katika sheria ya afya na usalama mahala pa kazi Sura ya 297.

Hata hivyo alieleza kwamba Tume inafanya tathmini ya utekelezaji wa sheria za mamlaka ya nchi kuhusu umilikimali na maliasili za nchi sura ya 449 pamoja na sheria ya mapitio na majadiliano  kuhusu masharti hasi katika mkataba wa mali asili na maliasilia  sura ya 450.

Eneo lingine ambalo limetajwa kufanyiwa tahmini ni katika utekelezaji wa sheria ya ugaidi sura ya 19 sambamba na utoaji wa elimu ya sheria kwa Umma na uandaaji wa machapisho pamoja na ushiriki wa maonesho mbalimbali hapa nchini alimalizia Katibu Mtendaji.

Kwa upande wake, Naibu Mwanasheria Mkuu Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Zanzibar, Bw. Shaaban Abdalla, alieleza kuwa ushirikiano huo unaongeza tija katika kazi za uhuishaji wa sheria kwa kuhakikisha kwamba mabadiliko ya kisheria yanayoletwa yanazingatia uhalisia wa jamii zote.

Tunaamini kuwa kazi za mapitio ya sheria zinahitaji ushirikiano wa karibu kati ya taasisi zote za kisheria katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Ushirikiano huu utasaidia pia kuondoa migongano ya kisheria na kujenga msingi wa sheria zinazotekelezeka kwa haki na usawa,alisema.

Katika kikao hicho, wajumbe walikubaliana pia kuunda kikosi kazi cha pamoja kitakachoratibu utekelezaji wa maeneo ya kipaumbele yaliyobainishwa katika MoU, ikiwemo masuala ya sheria za teknolojia, haki za binadamu, usuluhishi wa migogoro, na sheria za kimataifa zinazogusa pande zote za Muungano.

MoU kati ya Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Zanzibar ilisainiwa kwa lengo la kuimarisha ushirikiano wa kitaalamu, kubadilishana taarifa, na kujengeana uwezo katika nyanja mbalimbali za kisheria, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kuhakikisha maendeleo ya sheria yanaenda sambamba na mabadiliko ya kijamii, kiuchumi na kiteknolojia.

MWISHO

 

TUME YA KUREKEBISHA SHERIA YAPANGA MIKAKATI YA KUTEKELEZA DIRA YA TAIFA 2050





Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT) leo tarehe 7 Agosti, 2025 imeeleza namna ilivyojipanga kutekeleza Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2050 kwa kufanya maboresho katika mifumo ya sheria ili kuhakikisha inakidhi mahitaji ya vizazi vijavyo na kuendana na mabadiliko ya teknolojia, jamii na mazingira duniani.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma, Naibu Katibu wa Tume hiyo, Bi. Zainab Chanzi, alisema kuwa Dira ya Taifa ya 2050 ni dira pana na ya kipekee inayolenga kuiwezesha Tanzania kuwa Taifa jumuishi lenye ustawi, haki na linalojitegemea.

“Ili Dira ya 2050 iweze kufikiwa, sheria ni nyenzo muhimu katika utekelezaji wa Dira, hivyo sheria zetu lazima ziakisi misingi, nguzo na shabaha za Dira hiyo. Kama Tume, tumejipanga kuhakikisha sheria zinafanyiwa mapitio, tafiti na tathmini na wananchi kuelimishwa maboresho ya sheria kwa lengo la kujenga uelewa kwa wananchi,” alisema Bi. Chanzi.

Aidha Bi. Chanzi alibainisha mikakati mbalimbali ambayo Tume imepanga kutekeleza imiwemo kupitia Sheria zilizopitwa na wakati ili kuhakikisha hazikwamishi maendeleo ya kisasa kama vile matumizi ya akili unde (AI).

Akizungumzia kuhusu sekta ya Kilimo Bi. Zainab alieleza umuhimu wa Sekta ya Kilimo kwa kuwa kwa mujibu wa Dira 2050 ni miongoni wa sekta ya mageuzi hivyo kama Tume imejipanga kuhakikisha sheria zinazosimamia sekta hii zinaakisi matarajio yaliyowekwa na Dira kama vile kuwa Taifa linaloongoza katika uzalishaji wa chakula.


“Sheria tunazotunga leo ndizo zitakazojenga Tanzania ya baadaye. Hivyo basi, kazi yetu ni kuhakikisha msingi huo wa kisheria unawekwa kwa weledi, umakini na mshikamano wa kitaifa,” aliongeza.

Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Yatoa Elimu ya Sheria ya Ustawi wa W...

TAZAMA ELIMU YA MIRATHI ILIYOTOLEWA NA TUME YA KUREKEBISHA SHERIA MKOANI...


Mwanasheria Vicky Mbunde kutoka Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT),Baraka Chipamba, akitoa elimu kuhusu umuhimu wa kufungua mirathi baada ya marehemu kufariki wakati akizungumza na wananchi wa Kata ya Magomeni Bagamoyo mkoani Pwani Aprili 25, 2025.

 Bagamoyo

Mwanasheria Vicky Mbunde kutoka Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT), amesema kuandika wosia siyo uchuro bali unasaidia kuondoa migogoro ya kugombea mali zilizoachwa na marehemu.

Hayo yalibainishwa na mwanasheria huyo Aprili 25, 2025 wakati akizungumza na wananchi wa Kata ya Magomeni mjini Bagamoyo Mkoa wa Pwani wakati akitoa elimu inayohusu umuhimu wa kuandika Wosia pamoja na kujiepusha na makosa mbalimbali ya kimtandao.

Alisema makosa ya kimtandao yamekuwa yakifanyika kwa kutumia vifaa vya kielektroniki kama kompyuta, simu janja, vishikwambi na Teknolojia ya Mawasiliano ya Habari (TEHAMA).

Mbunde alisema wosia ni nyaraka ya kisheria ambayo inaonyesha matakwa na maagizo ya mtu kuhusu namna mali yake itakavyogawiwa baada ya kifo chake na kuwa unaweza kujumuisha maelekezo kuhusu jinsi mali itakavyogawiwa kwa warithi, uteuzi wa wasimamizi wa mali, na mambo mengine yanayohusiana na urithi wa mtu husika. 

" Malengo ya kuandika wosia ni kuhakikisha kwamba matakwa ya mtu yatatekelezwa ipasavyo baada ya kifo chake na kuwa unaweza kuwa na athari za kisheria na unaweza kutambulika na mahakama mara tu baada ya kifo cha mtu aliyeandika wosia huo," alisema Mbunde.

Mbunde alisema wosia unaweza kujumuisha mambo kadhaa, ikiwa ni pamoja na uteuzi wa warithi na kuonyesha ni nani atakayepokea mali za marehemu.

 Alisema mtu anaweza kuteua watu wa kusimamia mali zake na kutekeleza matakwa yake kama watekelezaji wa wosia ambao unaweza kuainisha jinsi mali inavyopaswa kutumika, kugawanywa, au kuhamishwa kifedha.


 
Mwanasheria wa Tume hiyo, Baraka Chipamba akizungumzia utaratibu wa kufungua mirathi alisema inategemeana kama marehemu aliacha wosia au hakuacha wosia.

 

Alisema kama marehemu aliacha wosia na kumchachagua mtu wa kusimamia na kugawa mirathi yake baada ya yeye kufariki, ataomba mahakamani kuthibitisha wosia huo.

 

Aliongeza kuwa kama hakuna wosia, hatua ya kwanza ni kuchagua msimamizi wa mirathi. ambaye ndugu wa marehemu watalipendekeza jina lake ili asimamie mirathi.

Alisema kazi ya msimamizi wa mirathi ni kufungua Mahakamani shauri la maombi ya kusimamia mirathi, kubainisha, kukusanya na kuhifadhi mali za marehemu, kulipa madeni yaliyoachwa na marehemu na kugawa kilichobaki kwa warithi halali.

 

Chipamba alisema siyo kila mahakama inaweza kusikiliza kesi hizo za mirathi ambapo amezitaja mahakama ambazozinasikiliza mashauri hayo kuwa ni Mahakama ya Mwanzo, Mahakama ya Wilaya. Mahakama ya Hakimu Mteule na Mahakama Kuu.

 

Alisema unaweza kwenda Mahakama ya Mwanzo kama mirathi inahusisha sheria za Kimila au za Kiislam  na hiyo haijalishi thamani na ukubwa wa mirathi husika hivyo kama wewe ni Mkristo, usiende Mahakama ya Mwanzo na utaenda Mahakama ya Mwanzo iwapo sheria inayotumika kwenye hiyo mirathi ni ya Kimila au Kiislam.

Aidha Chipamba alisema Mahakama ya Wilaya inasikiliza mashauri ya mirathi   ambayo haizidi Sh.100,000,000 kwa hiyo chochote chenye thamani ya kuanzia sifuri mpaka million mia ni  shauri dogo ambalo litasikilizwa.

 

" Usiende Mahakama ya Mwanzo, hata kama mirathi ni fedha ndogo. Utatakiwa kwenda  Mahakama ya iwapo tu sheria inayotumika ni ya kimila au kiislam," alisema Chipamba.

Mwanasheria Vicky Mbunde kutoka Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT),Vick Mbunde akitoa elimu kuhusu umuhimu wa kuandika Wosia kabla ya kifo wakati akizungumza na wananchi wa Kata ya Magomeni Bagamoyo mkoani Pwani Aprili 25, 2025.

Mwanasheria Vicky Mbunde kutoka Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT), Vick Mbunde, akigawa vipeperushi kwa wananchi wa Kata ya Magomeni wilayani Bagamoyo.

Afisa Mtendaji wa Kata ya Magomeni, Mwajuma Yombe, akizungumza wakati wa mafunzo hayo.
Mkazi wa Kata ya Magomeni, Tecra Philipo, akiuliza swali wakati wa utoaji wa elimu hiyo
Walimu wa Shule ya Sekondari ya Hassanali Damji wakishiriki kupata elimu ya sheria kutoka Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania.

Afisa Mtendaji wa Kata ya Dunda, Judith Mayunga, akitoa maelezo wakati wa utoaji wa elimu ya masuala ya mirathi wakati ilipokuwa ikitolewa kwa wafanyabiashara wa Soko la Samaki wilayani Bagamoyo.

Mwanasheria Vicky Mbunde kutoka Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT), Baraka Chipamba, akitoa elimu kuhusu umuhimu wa kufungua mirathi kwa wafanyabiashara wa Soko la Samaki Wilaya ya Bagamoyo.
Mwanasheria Vicky Mbunde kutoka Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania  (LRCT),Baraka Chipamba, akitoa elimu kuhusu umuhimu wa kufungua mirathi kwa walimu wa Shule ya Sekondari ya Hassanali Damji.
Wananchi wa Kata ya Magomeni wakipata elimu ya sheria kuhusu mirathi na kuandika wosia.
Elimu ikitolewa.
Mkazi wa Kata ya Magomeni, Seif Chama akiuliza swali.
Maswali yakiulizwa likiwemo matapeli wanawezaje kusajili laini za simu zaidi ya 100 wakati sheria hairuhusu?

Wananchi wa Kata ya  magomeni wakiwa wameshika vipeperushi vya Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania wakati wa upokeaji wa elimu hiyo.
Makamu Mkuu wa Shule ya Sekondari a Hassanali Damji, Jafari Mwandemo akizungumza wakati wa utoaji wa elimu hiyo.
Afisa Mtendaji wa Kata ya Magomeni, Mwajuma Yombe, akizungumza wakati wa utoaji wa elimu hiyo Shule ya Sekondari ya Hassanali Damji.
Viongozi wakiwa meza kuu wakati wa utoaji wa elimu hiyo Shule ya Sekondari ya Hassanali Damji.
Taswira ya utoaji elimu Shule ya Sekondari ya Hasanali Damji.

 Mkazi wa Kaole Selemani Iddi akiuliza maswali wakati wa mafunzo hayo.

Mwanasheria wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT), Vick Mbunde, akizungumza na Wanafunzi  wa Shule ya Sekondari ya Nyumbu wakati akitoa elimu ya sheria ya makosa ya kimtandao Kibaha Mkoa wa Pwani Aprili 24, 2025.

................................................... 

Na Mwandishi Wetu, Kibaha

TUME ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT), imeto elimu kwa wananchi zaidi ya Milioni 2 katika mkoa wa Pwani, Lindi na Mtwara inayohusu Sheria ya makosa ya kimtandao, maadili na ulinzi wa mtoto dhidi ya makosa hayo.

Mwanasheria wa Tume hiyo, Vicky Mbunde, akizungumza kwa nyakati tofauti Kibaha mkoani Pwani Aprili 24, 2025 wakati akitoa elimu kwa wanafunzi wa Chuo cha Walimu cha A3, Uuguzi na Uandishi wa Habari pamoja na wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Nyumbu aliwataka kuwa mabalozi na walinzi wa mtoto dhidi ya makosa ya kimtandao huku wakijiepusha kufanya makosa hayo.

Alisema makosa ya kimtandao yamekuwa yakitumika kwa kutumia vifaa vya kielektroniki kama kompyuta, simu janja na vishikwambi na Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA).

"Makosa hayo ni kurekodi picha mbaya za watoto kama za utupu, kufanyiwa vitendo vya ukatili, kudhalilishwa na vitendo vingine vinavyofanana na hivyo na kuzisambaza mtandaoni," alisema Mbunde.

Mbunde alisema mwanafunzi yeyote atakapoona vitendo hivyo vikifanyika au anafanyiwa atoe taarifa kwa walimu, wazazi na polisi ili wahusika waweze kuchukuliwa hatua za kisheria.

Alisema vitendo hivyo havikubaliki katika jamii na ndio maana zimetungwa sheria kali dhidi ya mtu yeyote atakayebainika kutenda makosa hayo.

Wakili Baraka Chipamba kutoka tume hiyo alisema makosa yote hayo yakiwepo ya ubakaji, kutia mimba na utoaji wa mimba adhabu yake ni kifungo cha zaidi ya miaka mitano nafaini kuanzia shilingi milioni tano hadi milioni 20 au zote kwa pamoja.

Walimu wa shule hizo waliipongeza tume hiyo kwakutoa elimu hiyo na wakaomba iwe endelevu kwani itasaidia kuwaondolea watoto hao madhira ambayo yanaweza kuyapata kutokana na vitendo hivyo.

Tume hiyo inatoa elimu hiyo chini ya Kaulimbiu isemayo Mabadiliko ya Sheria ni fursa ya kujenga taifa lenye haki na usawa kwa wote

Kuhusu Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania ni idara ya Serikali inayojitegemea chini ya Wizara ya Katiba na Sheria ambayo imeanzishwa kwa mujibu wa Sheria ya Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania, Sura ya 171, na ilianza kazi rasmi tarehe 21 Oktoba, 1983.  Kwa mujibu wa sheria, Tume ina jukumu la kufanya mapitio ya sheria zote za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili ziandane na mazingira ya wakati uliopo kwa maendeleo endelevu.Mwanasheria Baraka Chipamba kutoka Tume hiyo, akitoa elimu kwa wanafunzi wa Chuo cha Walimu cha A3, Uuguzi na Uandishi wa Habari.Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Nyumbu, Juma MMrope akizungumza wakati wa utoaji wa elimu hiyo.

Wanafunzi wa Chuo cha Walimu cha A3, Uuguzi na Uandishi wa Habari. wakipata elimu hiyo
Mwanasheria Vicky Mbunde, akisisitiza jambo wakati akitoa elimu kwa wanafunzi wa wa Chuo cha Walimu cha A3, Uuguzi na Uandishi wa Habari cha Kibaha mkoani Pwani.
Mwanasheria Baraka Chipamba kutoka Tume hiyo, akitoa elimu hiyo.
Wanafunzi wakiuliza maswali.
Picha ya pamoja 
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Nyumbu wakipata elimu hiyo.