HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

» » TUME ZA KUREKEBISHA SHERIA ZA TANZANIA NA ZANZIBAR ZASAINI MKATABA WA USHIRIKIANO.

 








TUME ya kurekebisha Sheria Tanzania na Ile ya  Zanzibar leo tarehe 12/07/2023 wamesaini Mkataba wenye lengo la kuboresha utendaji kazi katika tasnia ya sheria ambapo imeelezwa kwamba ushirikiano huo utasaidia kutatua changamoto mbalimbali za kijamii Mazingira na elimu.

Akiongea kabla ya kusaini mkataba huo Mwenyekiti wa Tume ya kurekebisha sheria Tanzania Jaji Msaafu wa Mahakama ya Rufaani Tanzania January Msoffe amesema Tume hizo zina maono na majukumu yanayofanana hivyo ushirikiano wao utaleta mabadiliko na tija makubwa.

Alisema kuwa ushirikiano kati ya Tume hizo utasaidia kuimarisha mfumo wa kisheria unaozingatia utawala bora na utawala wa sheria kwa maendeleo ya jamii.

"Ushirikiano huu utakuwa jukwaa muhimu la kubadilishana ujuzi, utaalamu na mbinu bora katika nyanja ya mageuzi ya sheria katika nchi, tutatumia nguvu zetu ili kuimarisha utafiti wa kisheria, mapitio na tathmini ya sheria zilizopo na kubainisha maeneo mbalimbali yenye changamoto na kujitahidi  kuondoa upungufu au mapengo yanayoweza kuwepo kati ya  mifumo ya sheria. "Amesema Jaji Msoffe.

Aidha amewataka wataalamu wa pande hizo mbili kuhakikisha wanaisoma na kuilelewa mikataba hiyo  ili waweze kuitekeleza kama inavyostahili ambapo ameeleza kwamba itasaidia kuoboresha utendaji kazi wao wa kila siku.

Kwa upande wake Mwenyeki wa Tume ya kurekebisha sheria Zanziba Khadija Shamte Mzee amesema mkataba huo ni dalili za kukua kwa taasisi hizo kwa kuwa tokea kuanzishwa kwake hazikuwahi kutokea.

Amezitaka taasisi hizo kuhakikisha zinabadilisha mitazamo hasi iliyopo kwa baadhi ya watu kwa kuonesha na kuyatangaza majukumu yao kwa jamii huku akielekeza Tume hizo kutoa tafiti kwenye shelfu na kuzibainisha kwa jamii kwa kuzifanyia kazi.

Mwenyekiti huyo ameendelea kueleza kwamba mashirikiano hayo yatapunguza gharama na uendeshaji wa majukumu ikiwemo utafiti uchapishaji wa majarida na ubadilishaji wa taarifa mbalimbali.

Ameongeza kuwa ni wakati wa kuongeza kasi ya utendaji kazi wao kwa kufanya mapitio ya sheria, kubadilisha mbinu na kuhakikisha  Tafiti zinakuwa ni Mali ya Jamii.

Akielezea mkataba huo, Katibu Mtendaji wa tume  Zanzibar, Mussa Kombo Bakari amesema mkataba huo una maeneo 10 ambayo ni kuimarisha ushirikiano baina ya tume hizo.

Pia kubadilishana taarifa ikiwemo ripoti za utafiti na nyaraka,  kufanya tafiti za pamoja, kubadilishana utaalamu na uzoefu baina ya pande zote.

 "Mkataba huu utaongeza utaalamu katika uandishi wa sheria na miswada. Itaundwa timu ya kuratibu na kutekeleza hati hii na kushauri, kuhakikisha usiri na mawasiliano," amesema Bakari.

Awali akieleza majukumu ya tume hizo Katibu Mtendaji wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Griffen Mwakapeje amesema  Kazi ya time hizo ni kufanya mapitio ya Sheria zote za Tanzania na Zanzibar  ili ziweze kuendana na Mazingira na jamii iliyopo.

Hata hivyo ameendelea kusema kwamba zipo sheria ambazo zinatakiwa kuondolea na  kwa kuwa zimekuwa za zamani na zipo ambazo zinatakiwa kusasishwa na na kufanya mapendekezo ya kutungwa Sheria nyingi kulingana Mazingira yaliopo.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Tuandikie Maoni yako