HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

» » Tume ya Kurekebisha Sheri yaanza mazoezi ya SHIMIWI









Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania imeanza mazoezi yake kuelekea  Mashindano ya Shirikisho la Michezo  ya Wizara na Idara za  Serikali (SHIMIWI) itakayofanyika  mkoani Iringa 27 Septemba 2023 .

Akizungumza  jana baada ya mazoezi hayo Katibu Mtendaji wa  Tume ya Kurekebisha Sheria  Griffin Mwakapeje  amesema wanamategemeo makubwa kwamba timu hiyo itafanya vizuri katika mashindano hayo.

Aidha Mwakapeje amewataka watumishi kujenga tabia ya kufanya mazoezi ili kuboresha na kulinda Afya  zao na kwamba hata mashindano hayo yatakapokwisha mazoezi yatandelee kufanyika kila jumanne na alhamisi.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Tawi la SHIMIWI Msafiri Shamsi Idd amesema timu hiyo inaendelea na mazoezi ya michezo mbalimbali ikiwemo Kuvuta Kamba, riadha, draft,bao na michezo mingine ambayo inatambuliwa na shirikisho hilo.

Amesema lengo la mazoezi hayo ni kuhakikisha kwamba Timu ina kuwa na utayari wa kimwili (fitness) pamoja na kujenga afya  jambo ambalo litasaidia Timu hiyo kutwaa ubingwa wa mashindano watakayoshiriki.

Adha amewataka washiriki wa michezo mbalimbali kuhakikisha wanafanya mazoezi kila siku ya jumanne na Alhamisi kama ratiba yao inavyonesha .

 

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Tuandikie Maoni yako