HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

» » » Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Mhe. Jaji Mstaafu January Msofe ahimiza utafiti wa sheria utakaowasaidia wananchi

 



Mwenyekiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Mhe. Jaji Mstaafu January Msofe amewataka watumishi wa Tume hiyo kujipanga na kuhakikisha wanaendelea kufanya mapitio na utafiti wa sheria zote nchini ili ziweze kuwanufaisha wananchi

Kauli hiyo ameitoa leo katika ukumbi wa mikutano wa Tume hiyo uliopo maeneo ya chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) alipokutana na watumishi wa Tume hiyo wakati wa kupata chakula cha mchana pamoja.

“Tume ina jukumu kubwa la kufanyia utafiti sheria zote hapa nchini na kupeleka mapendekezo sehemu husika hivyo jukumu hili linapaswa kuwa endelevu na kuonesha tija kwa taifa’ alisema Jaji Msofe.

Jaji Msofe amewataka wanasheria wa Tume hiyo kujipanga kikamilifu na kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao ya msingi yatakayosaidia sheria zinazotungwa kudumu kwa muda mrefu na kuwasaidia wananchi.

Aidha amewataka watumisha hao kuacha kufanya kazi kwa mazoea (business as ussual ) badala yake wajikite kufanya utafiti wa kina wa sheria mbalimbali ili kutimiza msingi wa kuanzishwa kwa Tume hiyo.

Yapo mapendekezo mbalimbali kuhusu maboresho ya sheria ya tume ya kurekebisha sheria, sasa ni lazima tuendelee kufanyia utafiti wa kina sheria mbalimbali kwani serikali inatutegeme,kila siku hakikisha unakuja na mbinu mpya  na wala tusifanye kazi as business as usual alisema jaji Msofe.

Jaji Msofe pia amewataka watumishi wa tume hiyo kuhakikisha wanashiriki mazoezi ambayo yanafanyika kila siku ya jumatatu na alhamisi ya kila wiki ili kujenga na kuimarisha afya zao na kuepuka magonjwa nyemelezi.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Tuandikie Maoni yako