HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

» » » TUME YA KUREKEBISHA SHERIA YAJIPANGA KULIPA KISASI SHIMIWI

 



























Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania michuoano ya  Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali ( SHIMIWI) inayofanyika Mkoani Iringa  baada ya kupata upinzani mkali kutoka timu ya kuvuta Kamba ya Wizara ya fedha wanaume na Wizara ya Ujenzi wanawake ambapo Tume ilishindwa michezo yote.

Akiongea leo baada ya kumalizika  mchezo Mwalimu wa timu hiyo Bw. Idrisa Juma Shabani alisema timu zimejithidi lakini bahati haikuwa upande wa Tume na kuwa ni sababu ya kupoteza  mchezo huo.

Idrisa ameendelea kusema kwamba kwasasa wanajipanga kwa mchezo mwingine wa siku inayofuata huku akitaja kupungukiwa wachezaji hasa wanawake ambapo kwa mchezo uliopita walilazimika kuvuta Kamba wakiwa pungufu (9 kwa 10) jambo ambalo ameeleza kwamba limechangia timu ya wanawake kukosa ushindi.

Hata hivyo amewataka wachezaji kutokata tamaa na kuendelea kufanya mazoezi ili kuzikabili michezo ya siku inayofuta ambapo ameeleza kwamba timu za mwaka huu zimejiandaa vizuri.

“tumepoteza michezo yetu miwili baina ya Hazina na Ujenzi, kwa upande wa wanaume tumeona ki mchezo tulikuwa tumezidiwa lakini kwa upande wa  wanawake walishindwa kwa sababu walikuwa pungufu, ni imani yangu kwamba kesho tutafanya vizuri zaidi kwa kuwa tutakuwa tumekamilika sehemu zote.”

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Tumesheria sport club Msafiri Shamsi Iddi amewataka wachezaji kupata muda wa kupumzika na kuyafanyia kazi baadhi ya makosa madogo yaliojitokeza na kufuata mafundisho ya mwalimu  ili kuhakisha wanapata ushindi katika michezo inayofuta.

Akiongea na mwandishi wetu  moja ya wachezaji  wa tumesheria sport club Azizi Hamisi Mbuni  ambeye pia ni katibu wa Timu hiyo anasema kushindwa kwa mchezo huo hakuwakatishi tamaa na wanauhakikka kwamba watafanyia mazoezi maelekezo ya mwalimu na kufanya vizuri katika michezo ijayo.














«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Tuandikie Maoni yako