HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

» » TUME YA KUREKEBISHA SHERIA TANZANIA YACHUNGULIA FAINALI ZA RIADHA –SHIMIWI 2023

 










Timu ya riadha ya Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania  imefuzu kwenda hatua ya robo fainali katika mchezo huo baada ya kushika nafasi ya tatu Katika mbio za urefu wa Mita  200 ambao umefanyika leo Katika uwanja wa Samora uliopo mjini Iringa  ikiwa ni  mashindano ya Wizara na Idara za Serikali (SHIMIWI)

Akiongea  baada ya mchezo huo Mwenyekiti wa timu  ya Tumesheria Bw. Msafiri Shamsi Iddi amesema nafasi hiyo imechukuliwa na mchezaji Respicious Rweymamu Kashero baada ya kupita washindani wake nane kutoka wizara na Taasisi mbalimbali waliokuwa wakishiriki mchezo huo.

Aidha ameeleza kwamba Kashero atashiriki  mbio hizo kwa mara nyingine mnano siku ya kesho tarehe  6/10/2023 kwa ajili ya mchezo wa nusu fainali ambao utakuwa ni mtoano.

Mwanyekiti huyo amesema   mchezo huo ni muhimu kwa kuwa ndio utakaosabaisha tumesheria  kusonga mbele Katika mchezo wa riadha au  kutolewa kwenye mashindano hayo.

Hata hivyo Msafiri ameendelea kusema  kwamba wachezaji wengine walioshiriki mchezo huo ni  Zakaria Kegoro ambaye alishiriki mbio za Mita 100 na kushika  nafasi ya tano (5) huku mkimbiaji mwingine Emmanuel masamu  akishiriki mbio za urefu wa Mita Mia nne(400) ambapo hakuweza kumaliza baada ya kupata maumivu kwenye misuli.

Msafiri alieleza kwamba mwanariadha  Bw. Emanuel Aidani Kayumbo ambaye alishiriki mbio mita 100 za wazee wa umri wa miaka kuanzia 55 ambapo alishika nafasi ya saba (7) baada ya kuanguka na kupata majeraha katika mguu wake wa kulia.

Katika hatua nyingine Timu ya kamba ya Tumesheria Sport Club inatarajia kuingia uwanjani kupambana na timu ya Bunge Siku ya Ijumaa tarehe 6/10/2023 ikiwa ni hatua za mtoano.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Tuandikie Maoni yako