HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

» » WAJUMBE WA BARAZA LA WAFANYAKAZI TUME YA KUREKEBISHA SHERIA WAFUNDWA KIGOMA

 









Wajumbe wa baraza la wafanyakazi la Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT) wametakiwa  kutimiza wajibu wao wa kushughulikia mipango ya Taasisi hiyo (planning ) utunzaji wa mali au bidhaa na kupokea au kujadili taarifa ya mapato na matumizi (budget) badala ya kutumia muda mwingi kulalamika au kukosoa viongozi huku wakikumbushwa  kuwa sehemu ya kuleta mabadiliko.

 

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Kigoma Salum Kalli kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa huo wakati wa kikao cha baraza la wafanyakazi  kilichofanyika tarehe 18.10.2023 katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya mkuu wa mkoa wa Kigoma ambapo ameeleza kwamba mikutano hiyo isitumike kama uwanja wa fujo kwa kulalamika au kukosoa viongozi pasipo kuwa na tija.

 

“Mada kuhusu Wajibu wa Wajumbe wa Baraza la Wafanyakazi ambayo itawasilishwa na Afisa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), ni muhimu sana kwani ikumbukwe kuwa bila kujua wajibu wao, wajumbe wanaweza kudhani kuwa jukumu lao kubwa ndani ya Baraza ni kulalamika, kulaumu, kushutumu, kukosoa na mambo mengine kama hayo hivyo, kufanya mikutano ya mabaraza iwe ni uwanja wa fujo badala ya kuwa mahala pa kushirikishana katika kujenga Tume yetu.” Alisema DC Salum.

Aidha DC Salum alibainisha kwamba Baraza hilo  lina dhima kubwa katika maendeleo ya taasisi hivyo kuwataka wajumbe  kuhakikisha wanajua majukumu yao ili kuwatendea haki watu  wanaowawakilisha.

“kuingia katika Baraza bila kujua jukumu lako la msingi ni sawa na wizi kama wizi wa aina nyingine hivyo kama mjumbe, utakuwa huwatendei haki wafanyakazi wenzako unaowawakilisha” alisema

Awali akimkaribisha mgeni rasmi Kaimu Katibu wa Tume hiyo Bw. Burhani Kishenyi amesema Mada mbalimbali zitajadailiwa ikiwemo taarifa ya Mabadiliko yaliyotokana na Maberosho Mbalimbali ya Kisera na Kisheria yaliyofanyika katika Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya.

 

Mada nyingine ni kuhusu Taarifa ya Utekelezaji kwa mwaka wa fedha 2022/2023 yaani kuanzia Julai, 2022 hadi Juni, 2023. Itakayojumuisha Mipango, Vipaumbele na Bajeti ya Tume katika mwaka wa fedha 2023/2024 ambapo amesema ni muhimu  kwa ustawi wa Tume  kwakuwa itasaidia kujitathmini katika utekelezaji wa majukumu ili kujua mafanikio, changamoto na sababu za changamoto hizo.

“Niseme wazi kuwa, mada hii ndiyo sababu ya msingi ya kufanyika kwa mikutano ya Mabaraza ya Wafanyakazi, ili kujua tulikotoka, tulipo na tunakokwenda kama Taasisi, kila mjumbe azingatie kikamilifu mada husika. Alisema Kishenyi

 

Hata hivyo Kishenyi alieleza kwamba Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania katika mwaka huo wa fedha ilipata Tsh Bilioni 4.66 ambapo milioni  730 ni  mishara  na Tsh. Bilioni tatu (3) ilikuwa kwa matumizi mengine.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Tuandikie Maoni yako