HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

» »Unlabelled » WATUMISHI TUME YA KUREKEBISHWA SHERIA WAHIMIZWA KUWAHUDUMIA WANANCHI

 




Watumishi Tume ya Kurekebisha sheria Tanzania wamehimizwa kuwahudumia wananchi ipasavyo ili kuwasaidia kuwa na uelewa juu ya masualala mbali mbali ya kisheria.

Rai hiyo imetolewa 26 januari 2024 na aliewahi kuwa katibu mtedaji Tume ya kurekebisha sheria Tanzania 2008-2011 Bw. Japhet Mojelwa Sagash alipotembelea banda la Tume hiyo katika maonesho ya wiki ya sheria yanayoendelea katika viwanja vya Nyerere Square Mkoani Dodoma.

Bw. Sagash alismea jamii inauhitaji wa huduma za kisheria na kwakua miongoni mwa majukumu ya tume hiyo ni kutoa elimu na kuchukua maoni ya wananchi na wadau hivyo iendelee na kasi ya kuwafikia wananchi ili kuwapa elimu ya kisheria.

“wafayakazi wa hii Tume nawahimiza wawafuate wananchi na wale wananchi wenye ufahamu juu ya tume nao waje kutoa maoni yao wasikae kusubiri kufuatwa” alisema Sagash.

Aidha katika hatua nyingine  Mstaafu huyo ameiomba wizara ya katiba na sheria kuitengea bajeti toshelezi Tume hiyo ili kuipa nguvu ya kuweza kufika sehemu zote za nchi kutekeleza jukumu la utoaji elimu ya sheria kwa umma.

“Naiomba Serikali kupitia wizara yetu ya katiba na sheria hii Tume ipewe kiasi cha Fedha cha kutosha kwa sababu kazi ya hii Tume ni utafiti wanatakiwa kuzunguka kila mahali hivyo lazima wawe na pesa ili wafike katika hayo maeneo wasipokua na pesa inakua vigumu kufanikiwa kuwafikia watu maeneo mbali mbali” alisisitiza Sagash

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Tuandikie Maoni yako