headlines

HABARI

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

» » Tume ya Kurekebisha Sheria iwe Taasisi inayojitegemea- Prof. Kabudi.
TUME SHERIA TANZANIA

 

Mwejikiti wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Jaji Winifrida Korosso akimkabidhi Taarifa nane (8) waziri wa katiba na Sheria Prof. Paramagamba Kabudi katika mkutano uliofanyika jana tarehe 16/10/2024 katika ukumbi wa wizara hiyo uliopo Mji wa Serikali Mtumba



Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT) imeshauriwa kufanya mageuzi ya kimuundo na kuwa Taasisi ya utafiti inayojitegemea ambayo itakuwa  chanzo cha fikra za kisheria cha serikali (think Tank) kama zilivyo taasisi nyingine za utafiti hapa nchini ili kuipatia uwezo mkubwa wa  kufanya tafiti na kutoa mapendekezo thabiti kwa ajili ya marekebisho ya sheria.

Ushauri huo umetolewa leo tarehe 16/10/2024 na Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Prof. Paramagamba Kabudi wakati wa mkutano wake wa kupokea  taarifa nane (8) za utafiti kutoka kwa tume hiyo, Makabidhiano yaliyofanyika  katika ukumbi wa mikutano wa Wizara hiyo ulioko mji wa serikali Mtumba.

Prof Kabudi amesema kwamba  kuifanya Tume ya Kurekebisha Sheria kuwa taasisi ya utafiti inayojitegemea kutaisaidia kuongeza uwezo wa taasis katika kuboresha ufanisi  na kuimarisha kazi zake.

Aidha ameeleza kwamba mageuzi ya kimuundo yanayoshauriwa yanakusudia kuhakikisha kuwa Tume hiyo inapata uhuru zaidi wa kufanya tafiti za kina juu ya sheria, na hivyo kutoa mapendekezo ya maboresho ya sheria kwa uhuru zaidi bila kuingiliwa na mamlaka nyingine.

Ikiwa Tume hii itakuwa taasisi huru ya utafiti, itakuwa kama taasisi nyingine za utafiti ambazo zinafanya kazi za kitaaluma na kutoa ripoti zilizo kamili na za kina kuhusu masuala mbalimbali ya kisheria. Alisema Prof. Kabudi.

Aidha, amesisitiza Tume hiyo kuanza kujiandaa kwa kuwasomesha wataalamu wake wa utafiti wa sheria ili waweze kuwa na elimu kuanzia ngazi ya uzamili na kuendelea ikiwa ni pamoja na kufuatalia kwa ukaribu maslahi yaliyobora kwa makamshna pamoja na watumishi wote  kwa ujumla.

Mageuzi haya yanaweza pia kuiwezesha Tume kuanzisha miradi ya utafiti yenye msukumo wa kitaaluma na inayoweza kuchangia katika maendeleo ya mfumo wa sheria nchini kwa ujumla.

 

«
Next
MKOA WA MANYARA WAFAIDI ELIMU YA SHERIA KUHUSU MAZAO YA UHALIFU -LRCT.
»
Previous
LRCT YAENDELEZA UTOAJI WA ELIMU KUHUSU MIGOGORO YA ARDHI KWA JAMII
Pages 21123456 »

No comments:

Tuandikie Maoni yako