HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

» » » Mabaraza ya wafanyakazi yatumike Kujenga Demokrasia sehemu za kazi - Kabudi



Mabaraza ya  wafanyakazi yanapaswa kutumika kama chombo muhimu katika kuboresha na kuimarisha demokrasia kwenye eneo la kazi badala ya kutumika pekee kukusanya na  kupitia maoni ya watumishi .


Kauli hiyo imetolewa tarehe 14/11/2024 na Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi katika ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Midland iliyopo mjini Dodoma wakati akifungua kikao cha 21 cha baraza la wafanyakazi la Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania ambapo ameleleza mabaraza hayo  yanahusisha ushirikishwaji wa wafanyakazi katika maamuzi ya Taasisi au shirika wanamofanyia kazi jambo ambalo  huongeza uwazi na uwajibikaji.

Waziri Kabudi ameipongeza Manejimenti ya Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania kwa kutimiza takwa la kisheria la kufanya kikao cha baraza huku akifafanua kwamba Baraza la Wafanyakazi halipaswi kuwa chombo cha kupokea malalamiko ya watumishi pekee ingawa ni muhimu kwa baraza hilo kushughulikia malalamiko na changamoto zinazowakabili wafanyakazi na badala yake  jukumu lake linapaswa kuwa pana zaidi. 

Prof amefafanua kwamba Baraza linaweza na linapaswa kuwa jukwaa la kuchochea maendeleo, kutoa maoni, na kutoa mawazo ya kuboresha ufanisi wa Taasisi kwa ujumla.

Demokrasia  katika eneo la kazi ni muhimu kwani inachochea ari ya kazi, kuimarisha ufanisi, na kujenga mazingira yenye amani na haki, alisistiza Waziri wa Kabudi.

“ Baraza la Wafanyakazi si tu chombo cha kusimamia haki za wafanyakazi, bali pia ni nyenzo muhimu ya kufanikisha malengo ya taasisi kupitia ushirikiano wa kweli na mawasiliano ya wazi” alisema Waziri 

Amesema  Baraza linatoa nafasi kwa wafanyakazi kutoa maoni, mawazo, na mapendekezo kuhusu masuala yanayohusu ustawi wao na maendeleo ya Taasisi kwa ujumla  hivyo kupitia Baraza la Wafanyakazi, viongozi watakiwa  kupata mawazo mapya ya kuboresha mazingira ya kazi.

Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa Tume hiyo Bw. George Mandepo, alieleza kwamba kikao hicho ni hitaji la kisheria na ni muhimu kwa kuwa linashirikisha  wafanyakazi katika michakato ya kufanya maamuzi ili kuimarisha ufanisi wa kazi.


Aidha amefafanua kwamba Tume inatekeleza mipango mbalimbali ya kuhakikisha kwamba watumishi wanapata mafunzo  ili kuwajengea uwezo na kuboresha ufanisi  katika kutekeleza majukumu yao.

Mkutano huo uliwaleta pamoja wafanyakazi wa Tume na wadau wengine muhimu kwa lengo la kujadili masuala ya kazi, kubadilishana mawazo, na kutafuta suluhisho la changamoto zinazokabili sekta ya sheria.


MWISHO

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Tuandikie Maoni yako