HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

» » Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania yashiriki kikamilifu maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani

 








Wanawake watumishi kutoka Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania wameshiriki maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani ambapo kimkoa yamefanyika katika viwanja vya Chinangari Park Jijini Dodoma.  

 Akizungumza mara baada ya maadhimisho hayo leo Machi 8,2025 Afisa Ugavi wa Tume hiyo Bi. Aneth Lyatuu amesema kuwa siku ya leo inawakumbusha na kuwapa ujasiri zaidi wa kuweza kusimamia malengo ambayo wamejiwekea katika akili zao. 

  "Siku ya leo niwaambie wanawake wenzangu tujitahidi kupendana ,mwenzako akikukasirisha mwambie, msamehe na tusonge mbele pia tutiane moyo na nguvu,"amesema.  

 Aidha amesema kupitia maadhimisho hayo wanawake wasisahau maadili ya watoto kwasababu wanawake ndiyo wanaoongoza jamii na inaanzia katika familia na wakisimama imara jamii yote itaimarika. 

  Maadhimisho ya siku ya Wanawake Duniani kitaifa yamefanyika Jijini Arusha ambapo yameongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.

«
Next
This is the most recent post.
»
Previous
Older Post

No comments:

Tuandikie Maoni yako