HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

» » MATUMIZI YA LUGHA YA KISWAHILI KATIKA SHERIA YATASAIDIA KUONDOA MIGOGORO KATIKA JAMII - GRIFFIN MWAKAPEJE.

 



Matumizi ya lugha ya kiswahili katika kutafsiri sheria za Tanzania yataongeza uelewa kwa wananchi na kuwasaidia kujua haki na wajibu wao katika utatuzi wa migogoro mbalimbali inayowakabili na kuongeza utii wa sheria bila shuruti.

Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mtendaji wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania Bw. Griffin Mwakapeje wakati akitoa wasilisho kuhusu mchango wa lugha ya kiswahili katika upatikanaji wa haki wakati wa kongamano lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Mount Meru iliyopo jijini Arusha.

Katibu huyo ameendelea kusema kwamba matumizi ya lugha ya kingereza badala ya lugha ya kiswahili kinachoeleweka na kutumiwa na wananchi wengi inawanyima  kufahamu na kuelewa sheria mbalimbali.

 Aidha Mwakapeje ameliomba Baraza la Kiswahili la Taifa (BAKITA) kuendelea na utafiti ili kupata misamiati muhimu itakayotumika katika sheria ili kuwaondolea ukakasi mahakimu na majaji kwa kuwa wanapata ugumu katika kuandika hukumu kwa lugha ya Kiswahili.

Bw. Mwakapeje amebainisha kwamba kwa sasa Tume ya Kurekebisha Sheria ipo katika utekelezaji wa jukumu la kutafsiri sheria na ripoti mabalimbali za kisheria  kutoka lugha ya kingereza kwenda lugha ya Kiswahili ili kuisaidia jamii kupata uelewa wa sheria hizo.

sisi tunapokwenda kutoa elimu kwa wananchi tunaona hitaji la sheria na machapisho mbalimbali kuwa kwa lugha ya Kiswahili ili kuwasaida kufanya rejea mbalimbali” Mwakapeje

Amesema pia Tanzania ina jumla ya sheria 550 ambapo kati ya hizo zilizotafsiriwa kwa lugha ya Kiswahili ni 246 ambapo bado juhudi zinaendelea kukamilisha zoezi hilo.

unaweza kuona sheria zilizotafsiriwa ni zaidi ya nusu lakini tumejipanga kuhakikisha kwamba zeezi linakamilika kwa wakati” Griffin Mwakapeje.

                                                                                                                                             

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Tuandikie Maoni yako