HABARI

  1. 1
  2. 2
  3. 3
  4. 4

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

» » SERIKALI KUENDELEA KUIMARISHA UTAFITI KUPITIA TUME YA KUREKEBISHA SHERIA- DKT. NDUMBARO
TUME SHERIA TANZANIA

 



Serikali imesema itaendelea kuimarisha na kutoa ushirikiano kwa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania ili  kuimarisha utafiti wa sheria mbalimbali hasa kipindi hiki ambacho Serikali imeamua kupeleka msaada wa kisheria kwa jamii.

Kauli hiyo imetolewa leo na Waziri wa Wizara ya Katiba na Sheria Dkt. Damas Ndumbaro wakati wa kufungua kongamano la huduma za msaada wa kisheria uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hoteli ya Mount Meru iliyopo mjini Arusha ambapo amesema  msaada wa kisheria unakwenda sambamba na utafiti wa sheria .

Dkt.Ndumbaro Amesema utafiti wa sheria ni muhimu kwa kuwa ndio unaotathmini ubora na uhalisia wa sheria kwa jamii jambo ambalo ameipongeza  Tume ya kurekebisha sheria Tanzania kwa namna wanavyokusanya maoni na wanavyopeleka elimu kwa wananchi.

Hata hivyo ameitaka Wizara ya Katiba na Sheria kuimarisha ushirikiano baina yao na Tume  pamoja na wadau wengine wa sheria  kwa kuwa sekta hiyo ni ya zamani lakini bado ni changa na inahitaji ushirikiano mkubwa.

Aidha Ndumbaro ameeleza kwamba ni muhimu Wizara yake  kuongeza ushirikiano baina ya Tume hiyo pamoja na wadau wengine ili kuweza kufanyia kazi mapendekezo yanayotolewa na wadau mbalimbali.

Aidha Ndumbaro ameeleza kwamba ushirikiano huo umesaidia katika utekelezaji wa kampeni ya msaada wa sheria “Mama Samia legal Aid campaign” iliyofanyika katika mikoa minne (4) ya Ruvuma,Tabora na Dodoma ambapo jumla ya watu 255,397 sawa na   watu 62,000 kwa kila mkoa  walifikiwa na kupatiwa huduma.

Hata hivyo ameelekeza kufanyika kwa  tafakuri ili kubaini changamoto zilizotokea wakati wa utekelezaji wa kampeni kwa awamu ya kwanza ya  utoaji wa huduma ya kisheria katika  mikoa hiyo  ili kuleta urahisi katika utekelezaji wa huduma hiyo kwa  awamu ya pili.

Katika hatua nyingine Dkt. Ndumbaro ametumia mkutano huo kutoa  msimamo wa serikali juu ya kukamatwa kwa Dkt. Slaa (Balozi) na wenzake watatu ambao wanashikiliwa na jeshi la polisi kwa tuhuma kwamba  wametumia vibaya uhuru wao wa kujieleza na kufanya uchochezi pamoja na uhaini kwa kuitisha maandamano na kutoa  kauli za vitisho dhidi ya Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Waziri huyo ameeleza kwamba serikali haiwezi kumfumbia mtu macho akatoa lugha zenye kugawa watu na kuhamasha vurugu kwenye nchi inayoendeshwa ki katiba na sheria na akaachiwa aendelee kuvunja amani badala yake atafikishwa mahakamani ili mahakama iweze kutoa maamuzi yake kulingana na walichokifanya huku akiwataka wanawatetea wajipange kwenda kutoa ushahidi mahakamani.

Hata hivyo aliendelea kusema kwamba hakuna uhusiano kati ya mkataba wa Bandari na kukamatwa kwao kwa kuwa wapo watu wengi watu wengi waliotoa maoni yao kwa nyakati tofauti na hawakukamatwa, kwa kuwa hawakuvunja sheria wakati wa kutuoa maoni yao.  

Aidha Ndumbaro amezionya Taasisi za Kimataifa ambazo zinatoa kauli zenye sura ya kulichafua taifa kuhusu swala hilo na kuwataka kuacha mara moja kwa kuwa nchi hii inaendeshwa kwa kufuata katiba na kisheria.

Mwisho

«
Next
MATUMIZI YA LUGHA YA KISWAHILI KATIKA SHERIA YATASAIDIA KUONDOA MIGOGORO KATIKA JAMII - GRIFFIN MWAKAPEJE.
»
Previous
KATIBU MTENDAJI TUME YA KUREKEBISHA SHERIA GRIFFIN MWAKAPEJE NA MCHANGO ...
Pages 21123456 »

No comments:

Tuandikie Maoni yako