HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

» » TUME YA KUREKEBISHA SHERIA NA MPANGO WA UTEKELEZAJI WA MAJUKUMU KIELEKITRONIKI

 



Tume ya kurekebisha Sheria Tanzania imeanza ujenzi wa mfumo wa kielektroniki wa utendaji kazi za Mapitio, Tathmini, na Utafiti wa Sheria mbalimbali za Tanzania bara utakarahisisha utekelezaji wa majukumu, kupunguza gharama, na kuboresha utunzaji wa kumbukumbu  za nyaraka.

Kauli hiyo imetolewa hivi karibuni na Katibu Mtendaji wa Tume hiyo Bw.Griffin Mwakapeje wakati akifungua kikao cha wataalamu wa TEHAMA kutoka Taasisi mbalimbali wakishirikiana na  wanasheria wa Tume hiyo, Mkutano  ulifanyika  katika ukumbi wa mikutano wa ofisi za Tume zilizoko Chuo kikuu cha Dodoma (UDOM).

Mwakapeje ameeleza kwamba mfumo huo utakaojulikana utakapokamilika utajulikana kwa jina la Law Reform Management Information System (LRMIS) utasaidia kurahisisha Mtiririko wa utendaji kazi (Business process), kufanya tathmini mbalimbali zitakazosaidia kubaini idadi ya mapendekezo ya Tume yaliyutumika katika maboresho au kuunda sheria mpya na utapunguza gharama wakati wa kuandika maandiko mbalimbali

“serikali imeridhia Uwepo wa mfumo huo na ni ukweli kwamba utawasaidia sana watafiti wetu katka utendaji kazi za Mapitio, Tathmini, na Utafiti wa Sheria mbalimbali i”

Akiongea wakati wa kikao kazi hicho Katibu huyo amewataka wataalamu hao kuhakikisha mfumo unaweza kuwasiliana au kushirikiana na mifumo mingine ili dhana ya kurahisha utendaji kazi iweze kupatikana kwa urahisi.

Aidha ameeleza kwamba kwa kutumia mfumo huo utasaidia kupunguza gharama na muda kwa kuwa utakuwa na uwezo wa kuwasiliana na mifumo mingine ya Taasisi za Kisheria ikiwemo mifumo ya Wizara ya Katiba na Sheria, Mwanasheria Mkuu wa Serikali pamoja na mifumo ya Mahakama.

Akimalizia hotuba yake Mwakapeje amesema kwamba Tanzania kuna sheria zaidi ya 450 ambazo wanapaswa kuzifanyia  mapatio ili kuona zinaendana na uhalisia katika mazingira ya sasa huku akibainisha kwamba kuna maeneo mengine mapya ambayo huibuka kila siku yanayohitaji kutengenezewa sheria.

Kikao hicho kitafanyika kwa muda wa siku kumi (10) na kitawahusisha wataalamu mbalimbali ambapo mfumo wa Mtiririko wa utendaji kazi (Business process) uliohuishwa utakuwa umepatikana pamoja na mahitaji mengine ya mfumo.

Mwisho

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Tuandikie Maoni yako