HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

» » TUMESHERIA WANAWAKE KUTUPA KARATA YAO YA MWISHO KESHO SHIMIWI 2023

 


TIMU ya kuvuta Kamba wanawake kutoka Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania leo imepoteza tena mchezo wake dhidi ya Wizara ya Utalii huku wakibainisha kwamba idadi ndogo ya  wachezaji walionao imechangia kupoteza mchezo huo.

Wakiongea kwa nyakati tofauti baada ya kumalizika kwa mchezo wa kuvuta Kamba uliokuwa ukifanyika katika viwanja vya Mkwawa mjini Iringa, wachezaji wa timu hiyo  wamesema walijiandaa vizuri lakini walizidiwa nguvu kwa kuwa walikuwa wachache ikilinganishwa na timu pinzani ambayo ilikuwa na wachezaji 10 huku wao wakiwa 9.

Hata hivyo walibainisha kwamba wamekuwa wakicheza pungufu kwa kuwa baadhi ya wachezaji wao walipata majeraha wakati wa mazoezi na wengine kupata udhuru jambo ambalo lilipunguza nguvu ya timu hiyo.

Aidha wachezaji hao wamewaomba watumishi wa Tume hiyo na wapenzi wote wa mchezo huo kuwaombea dua ili kupata ushidi katika mchezo unaofuata kwa kuwa wana mwalimu mzuri nguvu wanazo na mbinu mbalimbali za kupata ushindi.

Kwa upande wake Mwalimu wa timu hiyo Bw. Idrisa Juma Shabani alisema timu imejiandaa vizuri changamoto iliyotokea ni kuzidiwa nguvu na timu pinzania hivyo wanaendelea na mazoezi ili kuukabili mchezo wa unaofuata.

 

 

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Tuandikie Maoni yako