HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

» » TUMESHERIA YAPELEKA KILIO KWA RAS MBEYA - NI SHIMIWI 2023

 












Timu ya Kuvuta Kamba wanaume kutoka Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania leo imeibuka mshindi baada ya kuivuta timu ya RAS Mbeya kwa ushindi wa 1-0 katika mashindano ya Shirikisho la Michezo ya Wizara na Idara za Serikali ( SHIMIWI), mchezo uliofanyika katika viwanja vya Mkwawa Mkoani Iringa .

Katika mchezo wa kwanza timu zote zilimaliza kwa kutoshana nguvu na baada ya kuanza kwa kipindi cha pili cha mchezo, Tume sheria Sport Club waliweza kuibuka washindi kwa kuwavuta wapinzani wao katika dakika ya kwanza na sekunde 34.

Akiongea mara baada ya mchezo huo, Mwalimu  Idrisa Juma Shabani wa timu ya  Tume sheria Sport Club amewapongeza wachezaji wake kwa kufuata maelelekezo na kuwataka waendelee kuwa na ari kubwa ya mchezo ili kuweza kuingia hatua ya robo fainali ingawa tulipoteza mchezo wa jana.

“Tumeshinda lakini mchezo haukuwa mrahisi, wachezaji wamejituma kwa kiasi kikubwa unaweza kuona awamu ya kwanza tulitoa droo, tukabadilisha mbinu hatimaye tukapata ushindi,japo haikuwa kazi rahisi” alisema Mwalimu Idrisa.

Aidha Mwalimu ameelza kwamba mashindano hayo hayakuwa rahisi kwa kuwa timu zote zimejiandaa vizuri na kila timu ilitaka kujihakikishia kupata ushindi utakaofanya wasonge mbele  katika  mashindano hayo huku akibainisha  kwamba siri  kubwa ya ushindi walioupata ilikuwa ni umoja na mshikamano walioutengeneza .

Hata hivyo, ameeleza kwamba bado wameendelea kuwa na kibarua kigumu ambacho ambapo siku inayofuta watakuwa na mchezo mwingine mgumu ambao ni lazima washinde ili waweze kuendelea katika hatua ya robo fainali.

Kwa upande wake mchezaji wa nyuma katika mchezo huo (stopper) Bwana Japhace Tumaini  alipohojiwa ameeleza kwamba  mazoezi waliyoyafanya jana baada ya kupoteza mchezo wao na Wizara ya fedha  yaliwajenga  ikiwa ni pamoja na kubadilisha mbinu za uvutaji walizozipata kupitia kwa mwalimu wao jambo ambalo lilisababisha ushindi kupatikana.

Bw. Japhace amesema kwamba wanaendelea na mazoezi kwa lengo la kuhakikisha kwamba wanapata matokeao katika mchezo unaofuta ili timu iweze kuingia hatua ya nane bora.

Mwisho

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Tuandikie Maoni yako