HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

» » USULUHISHI NJE YA MFUMO WA MAHAKAMA WACHANGIA KUONGEZEKA KWA MAKOSA DHIDI YA MAADILI


 

Utafiti umebainisha kwamba usuluhishi wa makosa dhidi ya maadili  nje ya mfumo wa mahakama imekuwa ni sababu ya Kuongezeka kwa utendekaji wa makosa hayo kwakuwa Sheria ya Mwenendo wa Mashauri ya Jinai inaeleza kwamba makosa dhidi ya maadili Tanzania si miongoni mwa makosa yanayoweza kusuluhishwa nje ya mahakama.

Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa Tume ya kurekebisha sheria Tanzania Jaji Mstaafu January Msofe wakati  akiwasilisha taarifa za mapitio ya mfumo wa sheria zinazosimamia makosa dhidi ya maadili Tanzania na taarifa ya mapitio ya mfumo wa sheria zinazosimamia udhamini Tanzania.

 

Jaji Msofe amesema kwamba utafiti umebaini kuwa sehemu kubwa ya jamii ya Tanzania inasuluhisha makosa hayo katika ngazi za familia, taasisi za dini, Serikali za Mitaa au Mabaraza ya Kata Ingawa Sheria ya Mwenendo wa Mashauri ya Jinai inaeleza bayana kwamba makosa dhidi ya maadili Tanzania sio miongoni mwa makosa yanayoweza kusuluhishwa nje ya mahakama.

 

sababu nyingine inayochangia kuongezeka kwa utendekaji wa makosa dhidi ya maadili ni usuluhishi wa makosa hayo nje ya mfumo wa mahakama. Ingawa Sheria ya Mwenendo wa Mashauri ya Jinai inaeleza bayana kwamba makosa dhidi ya maadili Tanzania si miongoni kwa makosa yanayoweza kusuluhishwa nje ya mahakama, utafiti umebaini kuwa sehemu kubwa ya jamii ya Tanzania inasuluhisha makosa hayo katika ngazi za familia, taasisi za dini, Serikali za Mitaa au Mabaraza ya Kata” Jaji Msofe.

 

Naye Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Pindi Chana wakati wa kikao hicho ameipongeza tume hiyo kwa kutekeleza majukumu yake kwa ufasaha jambo ambalo ameeleza kwamba linachangia kuimarisha Amani na utulivu nchini.

 

Aidha amewataka Watanzania kutumia madawati maalumu ya huduma ya msaada wa sheria unaotolewa katika ngazi za kata Wilaya na Mkoa ili wapate elimu na waweze kutatua changamoto zinazowakabili huku wakitakiwa kutokuwa waoga kuomba kuelimishwa kuhusu changamoto zinazowakabili na namna ya kuzitatua.

 

 

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Tuandikie Maoni yako