HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

» » TUME YA KUREKEBISHA SHERIA TANZANIA YAPONGEZWA KWA KUWAFUATA WADAU NA KUTOA ELIMU YA SHERIA MKOANI RUKWA

 




KATIBU Tawala Mkoa wa Rukwa Gerald Kusaya ameipongeza  Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT) kwa uamuzi wake wa kutoa elimu kuhusu sheria mbalimbali  Katika shule za msingi na sekondari Mkoani hapo kwa na lengo la kuongeza uelewa wa sheria na utii wa sheria bila shuruti.

 

Ametoa pongezi hizo leo tarehe 21/11/2023 ofsini kwake baada ya kukutana na ujumbe kutoka Tume hiyo ambao walimfahamisha kwamba wapo Mkoani hapo kwa lengo la  kutoa elimu ya sheria kwa wanafunzi wa shule  za msingi na Sekondari.

 

Bwana Kusaya amesema zoezi hilo litakuwa na  tija kubwa kwa jamii kwa kuwa jamii ina uhitaji mkubwa wa elimu ya sheria. Aidha, ameeleza kwamba  elimu hiyo itawasaidia watoto kufahamu haki na wajibu wao na kujiepusha kutenda makosa mbalimbali yaliyoanishwa katika sheria husika.

 

" Niwapongeze kwa uamuzi wa kutembelea wanafunzi na kuwapa elimu ili watambue haki na wajibu wao katika jamii, kwa kweli huduma yenu inahitajika sana Mkoani hapa" alisema Kusaya.

Aidha, Katibu Tawala huyo ameiomba Tume ya Kurekebisha Sheria  kuendelea kutoa elimu hiyo kwenye shule na vikundi mbali mbali vya vijana na wajasiriamali kwa kuwa uelewa wa sheria utasaidia wananchi kutii sheria bila shuruti.

Hata hivyo Kusaya ameshauri elimu hiyo kuendelea kutolewa katika makundi mbalimbali ya jamii na bila kusuburi watende makosa na kufikishwa mahakamani.

Awali akitoa maelezo ya utambulisho Mkuu wa Kitengo  Cha Elimu ya Sheria kwa Umma, Naibu Katibu Mtendaji, Bi Zainabu Chanzi amesema miongoni mwa majukumu ya Tume hiyo ni kutoa elimu kwa umma ili kuisaidia jamii kuzielewa Sheria mbalimbali na kupunguza utendekeji wa makosa mbalimbali  ya jinai.

Elimu iliyotolewa ni kuhusu Sheria ya Mtoto,Makosa dhidi ya Maadili ya Utu,Makosa ya Kimtandao, Sheria ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya, Ziara hiyo itachukua muda wa siku mbili na shule mbalimbali za Manispaa ya Rukwa zipata huduma hiyo.

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Tuandikie Maoni yako