HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

» » Kamati ya Bajeti ya Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania yakutana












Kamati ya  Bajeti ya Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania leo imekutana Jijini Arusha katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Hazina Ndogo  kwa lengo la kuandaa Mpango na Bajeti ya Tume kwa mwaka wa fedha 2024/25 ambao utasaidia  kuendesha shughuli za Taasisi hiyo.

Akiongea katika ufunguzi wa Kamati hiyo Naibu Katibu kwa niaba ya Katibu Mtendaji, Bw.Burhani Kishenyi amesema Mpango na Bajeti ujielekeze katika kuimarisha shughuli za mapitio, tathmini, utafiti na elimu ya sheria kwa umma kwa kuzingatia Mpango wa Maboresho  ya Sheria na utekelezaji  wa masuala ya Haki Jinai.

Bw. Kishenyi ameeleza kwamba utekelezaji wa  Mpango na Bajeti ni muhimu ukajielekeza katika matumizi ya TEHAMA pamoja na kuendeleza rasilimali watu kwa kuwajengea uwezo watumishi kwenye mafunzo ya muda mfupi na mrefu.

Aidha ameeleza kwamba utekelezaji wa Mpango na Bajeti utajielekeza kwenye matumizi ya mifumo mbalimbali ikiwemo  Mfumo wa manunuzi  (NeST) na Mfumo wa Kupima Utendaji Kazi wa Watumishi wa Umma na Taasisi ( PEPMIS).

Kwa upande wake Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mipango na Uratibu Bi. Fatma Alawi amesema kikao hicho kitasaidia kuwajengea uwezo maafisa wa bajeti katika usimamizi na ufuatiliaji wa kazi.

 


«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Tuandikie Maoni yako