HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

HABARI

» » » Watumishi watakiwa kujifunza mifumo ya uendeshaji wa Serikali

 


















Wakuu wa Vitengo wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania (LRCT) wametakiwa kujifunza mifumo yote ambayo Serikali inaitumia katika utekelezaji wa shughuli zake ikiwemo mfumo wa manunuzi (NEST, ESS) kwa kuwa Serikali imehamia kwenye mifumo ya kielekitroniki.

Maelekezo hayo yametolewa  leo tarehe  9/01/2024 na Katibu Mtendaji wa Tume hiyo George  Mandepo  wakati wa kikao cha Menejimenti kilichofanyika kwenye ukumbi wa mikutano wa ofisi hizo ambapo aliagiza kila Mkuu wa Kitengo kujifunza mifumo iliyoandaliwa na Serikali ili kusaidia utekelezaji wa shughuli za kila siku zikiwemo  za manunuzi.

kila mkuu wa kitengo ahakikishe anajifunza mifumo iliyopo ili asikwame kutoa huduma, Serikali imehamia kwenye utumiaji wa mifumo ya elekitroniki ambapo huwezi kununua chochote nje ya mfumo, na utekelezaji wa majukumu yetu unategema mifumo hiyo. ” George Mandepo.

Katibu Mtendaji ameelekeza kutafutwa wataalamu wa mifumo ambao watatoa mafunzo kwa watumishi wote wa Tume kwa wakati ili kuboresha utendaji kazi.  

Hata hivyo ameelekeza kamati za mafunzo  kutekeleza majukumu yake kwa kutoa  mafunzo maalumu kwa madereva ikiwa ni pamoja na elimu ya utambuzi pindi panapokuwa na magari mapya ya ofsini.

 Aidha, amewataka watumishi kujenga utamaduni wa kutunza vitendea kazi yakiwemo magari huku akitaka akiwakumbusha madereva  kutii sheria za barabarani bila shuruti ili kuepusha ajali na uharibifu wa mali za serikali.

Mwisho

 

«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Tuandikie Maoni yako