Watumishi wa Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania
wametakiwa kujenga mazoea ya kuandika taarifa baada ya kukamilisha kazi na
baada ya kumaliza Mafunzo kwa
wanaohudhuria ili kujenga uelewa
wa pamoja Katika Taasisi.
"Wapo watu wanaenda Mafunzo ya muda mfupi na mrefu na wengine
wakiwa wanasafiri sehemu mbalimbali kwa ajili ya kufanya kazi lakini wakirejea
Ofisini hawaandiki taarifa ya walichojifunza
(back to office report).
Aidha amehimiza kila mtumishi ambaye atakwenda safari ya kikazi au Mafunzo ndani
na nje ya nchi au vikao vya nje ya ofisi wanapaswa kuandika taarifa kueleza
yaliojiri na kuonesha mapendekezo
kulingana na changamoto zilizojitokeza.
Kwa upande wake Naibu Katibu Mtendaji Zainab Chanzi,
amewataka watumishi hao kuongeza juhudi ya kujifunza kutoka kwa wenzao wenye
ujuzi ili kuweza kuhamishia ujuzi kutoka mtumishi mmoja hadi mwingine.






No comments: